Sunday 1 September 2013

IGP ASAFISHA VIGOGO UWANJA WA NDEGE.

Dar es Salaam. Siku chache baada ya kuibuliwa kwa kashfa ya kupitishwa kiholela kwa dawa za kulevya katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Jeshi la Polisi limemwondoa Kamanda wa Polisi wa Viwanja vya Ndege Kamishna Msaidizi (ACP), Deusdedit Kato pamoja na Mkuu wake wa Upelelezi, David Mwafwimbo.
Mbali ya maofisa hao, pia jeshi hilo limemwondoa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Linus Sinzumwa, naye ikiwa ni miezi michache baada ya kutokea kwa ghasia wakati baadhi ya wakazi wa huko walipokuwa wakipinga mpango wa Serikali wa ujenzi wa bomba la gesi kwenda Dar es Salaam.
Nafasi ya Kamanda Sinzumwa imechukuliwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Zelothe Stephen kutoka Makao Makuu ya Polisi.
Taarifa iliyotolewa jana na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Senso ilisema Mkuu wa jeshi hilo, Inspekta Jenerali (IGP), Said Mwema amemteua, ACP Selemani Hamisi kuchukua nafasi ya Kato ambaye anahamishiwa makao makuu ya jeshi hilo. Kabla ya uteuzi huo, Kamanda Hamisi alikuwa Makao Makuu Idara ya Upelelezi.
IGP Mwema pia amemteua Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Hamad Hamad kuchukua nafasi ya Mwafwimbo aliyehamishiwa mkoani Lindi kuwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Lindi (OCD).
Taarifa hiyo ya Polisi ilisema uhamisho huo ni wa kawaida kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo yake. Hata hivyo, katika siku za karibuni, kumekuwa na malalamiko mengi kuwa vyombo vya usalama katika uwanja huo vimeshindwa kudhibiti biashara hiyo na matokeo yake Tanzania imechafuka katika medani ya kimataifa kutokana na idadi kubwa ya vijana wake kukamatwa sehemu mbalimbali duniani.
Matukio ya karibuni yanahusisha kukamatwa kwa wasanii Agnes Masongange na Melisa Edward waliokamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo, Johannesburg, Afrika Kusini.
Kutokana na kashfa hiyo, Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe aliamua kulivalia njuga suala hilo na kuchukua hatua kadhaa na pia alifichua jinsi wasichana hao walivyosaidiwa kupitisha dawa hizo na mtandao uliohusisha polisi, maofisa usalama wa taifa na baadhi ya wafanyakazi wa JNIA.
RPC Mtwara
Sinzumwa anaondoka Mtwara baada ya ghasia kubwa zilizozuka Mei mwaka huu wakati baadhi ya wakazi wa Mtwara walipokuwa wakipinga gesi kutoka Msimbati kusafirishwa kwa bomba hadi Dar es Salaam.
Katika ghasia hizo, ambazo Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), liliingilia kati, polisi walishutumiwa na wakazi wa huko kwa kutumia nguvu kubwa na kuwasababishia madhara.
Mwananchi



 President Jakaya Mrisho Kikwete walks with  Ms Kristalina Georgieva, the  European Commissioner for International Cooperation and Humanitarian Aid, shortly before the start of the High-level Retreat on "New Ideas for a Fair Globalization in Alpabch, Austria August 30, 2013.
 President Jakaya Mrisho Kikwete walks with Dr Jeffrey Sachs, Director of Earth Institute at the Columbia University, as they head to the meeting hall to  attend the High-level Retreat on "New Ideas for a Fair Globalization in Alpabch, Austria August 30, 2013.
President Jakaya Mrisho Kikwete with Mr Manuel Jose Barroso, President of the European Commission, at the start of the High-level Retreat on "New Ideas for a Fair Globalization in Alpabch, Austria August 30, 2013.
President Jakaya Mrisho Kikwete attends the High-level Retreat on "New Ideas for a Fair Globalization in Alpabch, Austria August 30, 2013. Left are members of his delegation, Professor Rwekaza Mukandala, Vice Chancellor of the University of Dar es salaam and Profesor Joseph Semboja, Principal Uongozi Institute.
 President Jakaya Mrisho Kikwete attends the High-level Retreat on "New Ideas for a Fair Globalization in Alpabch, Austria August 30, 2013. Right is the host and Co-Chairman of the Retreat, Mr Manuel Jose Barroso, President of the European Commission, followed by Ms Valerie Amos, UN Under-Secretary-General of for Humanitarian Affairs and Emergency Relief Coordinator
State House Photos