Friday 19 February 2016

KITUO CHA MABASI MASASI SASA SAFI, WAHUSIKA WAAMKA BAADA YA KUMULIKWA (+VIDEO)
Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo Mikoani Wilayani Masasi yaendelea Kuboreshwa kwa kufanyiwa Usafi wa Hali yajuu.

Leo hii Baada ya Kamera ya Lindiyetu.com kupita majira ya asubuhi ilikuta eneo hilo ambalo hapo jana lilikuwa limetapakaa Uchafu wa Kila aina likiwa Safi Kabisa.

KAMA ULIPITWA NA POST HIYO BOFYA HAPA KUANGALIA UCHAFU ULIOKUWEPO 



Hii inaonesha kabisa Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Masasi amedhamiria kuepuka aibu ambayo ilikuwa inakuja siku za usoni kwani eneo hilo lipo katikati ya Mji huo hivyo kuonekana kirahisi na Kuleta Picha mbaya.


Tunaipongeza Halmashauri ya Mji ambayo imelichukua jambo hili kwa Umakini mkubwa hadi kufikia Kuweka Greda ambalo lilikutwa likifanya kazi ya kuendelea kuweka Mazingira sawia katika Stend kuu hiyo.

UNAWEZA BOFYA PLAY KUTAZAMA VIDEO HAPO CHINI
HONGERENI SANA...!!!

Thursday 18 February 2016

JUKWAA LA BIOTEKNOLOJIA LATOA MAFUNZO KWA WALIMU WANAFUNZI WA CHUO CHA BUNDA KUHUSU BIOTEKNOLOJIA
Mtafiti Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania na Mkufunzi wa Mafunzo ya Bioteknolojia , Dk.Emmarold Mneney (kulia), akiwafundisha wanachuo wa Chuo cha Ualimu cha Bunda (BUNDA TTC), kuhusu matumizi ya bioteknolojia na uhandisi jeni Wilaya ya Bunda mkoani Mara leo asubuhi.
Mtafiti Kiongozi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk.Nicholaus Nyange (kulia), akizungumza na wanachuo hao katika mafunzo hayo.
Wanachuo hao wakifuatilia mafunzo hayo. 


Mtafiti Kiongozi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk.Nicholaus Nyange (kushoto) na Mkuu wa Chuo hicho, Rweyemamu wakiwa katika mafunzo hayo.
Walimu wa chuo hicho wakifuatilia mafunzo hayo.
Wanafunzi wakiwa katika mafunzo

Wanachuo hao wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo
Mwanachuo, Noshad Bryson akiuliza swali katika mafunzo hayo.
Mwanachuo, Mahana Mahana akiuliza swali.
Mwanachuo, Elias Yohana akiuliza swali.
Hapa baada ya mafunzo ni msosi kwa kwenda mbele.

Na Dotto Mwaibale

JUKWAA la Bioteknolojia Tanzania limetoa mafunzo ya matumizi ya bioteknolojia na Uhandisi Jeni kwa wanachuo cha ualimu Bunda kilichopo mkoani Mara ili kuwa jengea uwezo wa kuielewa teknolojia ya bioteknolojia  kwa ajili ya kusaidia kukabiliana na changamoto za kilimo.

Akizungumza na wanafunzi hao jana Mtafiti Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech) Dk. Emmalord Mneney alisema kuwa teknolojia hiyo mpya ni muhimu kusambaa nchini ili kumkomboa mkulima.

"Tumeamua kuleta mafunzo haya kwa wanachuo hiki tukiamini kuwa baada ya kuhitimu mafunzo yao watakwenda kuwaelimisha wakulima katika maeneo yao"alisema Dk. Mneney.


Dk.mneney aliongeza kuwa kutokana na kuwepo kwa changamoto ya tabianchi kumesababisha ukame na uharibifu wa mazingira ambayo yameathiri shughuli za kilimo hasa mazao.

Alisema kuwa kutokana na hali hiyo serikali imekuwa ikiiwezesha Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech) kwa ajili ya kuwaongezea uwezo wa kufanya tafiti za kilimo nchini.

Dk.Mneney alisema kuwa changamoto kubwa ya wakulima ni kukosa mbegu bora za mazao ya pamba na mahindi hali iliyosababisha wakulima wengi kukata tamaa ya kilimo hicho na kuamua kulima mazao mengine.

"Kutokana na changamoto hiyo Costech imekuwa ikifanya utafiti ndani ya maabara ya kisasa iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam ili kupata mbegu bora ambazo zikionekana kuwa zinafaa zitasambazwa katika mashamaba makubwa na nchi nzima kwa ujumla" alisema Dk.Mneney.


Mwanachuo hicho Mahana Mahana alisema mkoa wa Mara unachangamoto kubwa ya kilimo kutokana na ardhi kuchoka hivyo ni wakati wa watafiti kuliangalia hilo ili kuwasaidia wakulima kupata mbegu bora zitakazo waletea mafanikio ya kilimo ya kupata mazao mengi.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)





Dar es Salaam, Februari 17, 2016 - Fastjet imepunguza mtiririko wa safari zake  kwenye njia ya Kilimanjaro Tanzania na Nairobi Kenya kuanzia Jumatatu Februari 15, 2016.
Fastjet ambao awali walikuwa wanatoa safari za kila siku kwenye njia hii hivi sasa watakuwa wanafanya  safari kutoka Uwanja Ndege wa  Kimataifa wa Jomo Kenyatta hadi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro mara mbili kwa wiki  siku za Ijumaa na Jumapili tu.
Mabadiliko ya  mtiririko wa safari utazifanya ndege za fastjet kuondoka Nairobi kila Ijumaa na Jumapili saa 5.40 na kutua Kilimanajaro saa 6.40 na safari ya kurudi ndege itaondoka Kilimanjaro saa 7.10 na kutua Nairobi saa 8.10.

Kupunguzwa kwa safari hizo kumetokana na kuwepo kwa mahitaji kidogo miongoni mwa wateja nyakati za wiki kutoka masoko yote mawili ya Kilimanjaro na Nairobi na hivyo kufanya safari za ndege za kila siku kutokuwa nzuri kibiashara  kwenye siku hizo.
Shirika hilo limesema kuwa lengo lake ni kurejesha safari hizo kwenye njia ya Kilimanjaro –Nairobi pindi tu wateja wake watakapohitaji.


Safari za kila siku za  kutoka Dar es Salaam na Kilimanjaro hadi Nairobi zilianza Januari 11, 2016.
Mahitaji ya abiria kwa safari za ndege kwenye njia kubwa ya kibiashara kati ya majiji ya Dar es Salaam na Nairobi   ambayo kwa pamoja  yana idadi ya watu zaidi ya milioni nane yamekuwa ni ya kuridhisha na fastjet iko kwenye mawazo kuwa  ndege moja ni lazima iongezeke kwenye safari kati ya majiji haya miwili katika siku za usoni.

Matokeo ya safari za fastjet kwenda Nairobi kutoka Dar es Salaam yamekuwa ni makubwa ambako kunaelezwa na ukweli kuwa nauli zinazotolewa na mashirika ya ushindani kati ya  nchi hizo mbili zimeshuka kwa  kiwango cha hadi asilimia 40 tangu fastjet waanze safari zake.
Nauli za fastjet kwa kiwango kikubwa zipo chini kuliko zile zinazotozwa na mashirika mengine  kwa safari za moja kwa moja kati ya Nairobi/Dar es Salaam  ambapo nauli zinaanzia dola 80 kwa safari moja.

Nauli hizo hazijumuishi kodi ya serikali ambayo ni dola 49 kuondokea Tanzania na dola 40 kuondokea Kenya na hivyo fastjet kupendekeza wateja wake kufanya maandalizi mapema ili kutumia fursa hiyo ya tozo la nauli nafuu.



Hata hivyo fastjet inasisitiza kuwa  kupunguza safari kwenye njia kati ya Nairobi na Kilimanjaro kunafungua fursa ya kuongeza uwezo kwenye njia za kikanda zilizopo na hali kadhalika uwezekano wa kuzindua  njia nyingine mpya ya kikanda katika siku za karibuni.

Wednesday 17 February 2016

AU Commission urges African governments to use commodity downturn to strengthen their laws and institutions

Cape Town, South Africa, 7 February 2016 (ECA) – A keynote speech delivered on behalf of Her Excellency Mrs Fatima Acyl, African Union Commissioner for Trade and Industry at Cape Town’s annual Mining Indaba acknowledged the reality of the commodity price slump, but also identified the opportunity for African governments to create the right legal and institutional framework to drive change in their economies.

“Now that the boom is over, it is even more imperative for all stakeholders to get down to the hard work of implementing the development agenda embodied in the African Mining Vision, for sustainable structural transformation of African economies,” urged Her Excellency in the speech.

Stressing that the Africa Mining Vision (AMV) went well beyond simply questions of taxes and revenue collection, the Commissioner’s speech stressed mining’s role in linkages and infrastructure development.

“A typical mining company spends over 61 percent of its total investment on infrastructure and procurement – more than three times what is paid in taxes,” noted the Commissioner’s speech. “Investment through linkages presents opportunities for governments to align their development policies in ways that capture greater value from mining,”

The speech was delivered at the annual Ministerial Symposium, held the Sunday before Mining Indaba commences. The Symposium provides a platform for ministers responsible for mineral resources to discuss common risks and opportunities associated with the implementation of the Africa Mining Vision. 
CODES NA LINK: LINK: https://soundcloud.com/issamichuzi/balozi-ombeni-sefue-siku-100-za-rais-magufuli-feb-122016

Mkuu wa  Kitengo cha Vifaa vya Mawasiliano wa TigoDavid Zakaria akielezea athari  za matumizi ya  simu bandia kwa waandishi wa habari  (Hawapo pichani) katika mkutano uliofanyika mapema leo katika makao makuu ya Tigo Kijitonyama Dar es salaam., kushoto kwake ni Meneja wa Mawasiliano, John Wanyancha


Dar es Salaam, Februari 16 2016 - Watumiaji wa simu za mkononi wameonywa dhidi ya matumizi ya simu bandia na zisisokidhi viwango vya ubora ambazo tayari zimetangwa kupigwa marufuku na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuanzia mwezi Juni mwaka huu.
Kutokana na sababu hiyo, Tigo, ambayo ni kampuni ya kidijitali, imeanza kuendesha kampeni ya kuhamasisisha wateja wake na umma kwa jumla kupitia vyombo vya Habari inayolenga kuwaepusha na athari za matumizi ya simu bandia.

 ``Kwa mujibu wa maelekezo ya TCRA matumizi ya simu za mkononi ambazo namba zake za utambulisho wa kimataifa (IMEI) ni bandia yatapigwa marufuku kutumika kwa mitandao yote ya simu nchini Tanzania kuanzia Juni 16 mwaka huu. Ili kujiepusha na usumbufu wowote utakaotokana na hatua hii tunawashauri wateja wetu kujipatia simu halisi na bora kutoka maduka ya Tigo yaliyo karibu nao,`` alisema Mkuu wa  Kitengo cha Vifaa vya Mawasiliano wa Tigo, David Zakaria.
Ripoti ya utafiti ulichapishwa katika tovuti ya GSMA ("http://www.gsma.com" www.gsma.com ) inasema kwamba tofauti na ilivyo kwa simu halali ambazo hupitia mamia ya hatua mbalimbali za kuhakiki ubora wake kabla ya kupelekwa sokoni, simu bandia hazifanyiwi majarbio ya ubora na kuna taarifa za kitafiti zinazoonyesha kuwa baadhi ya simu bandia zina kiwango kikubwa cha madini ya risasi na vitu vingine ambavyo ni hatari kwa mazingira na afya ya binadamu.
Ripoti hiyo inaendelea kusema kuwa simu feki zinatengenezwa na malighafi dhaifu zisizokidhi viwango na zimeshaonesha kuwa kiwango cha hatari cha vyuma na kemikali kama risasi hadi kufikia kiwango cha mara 40 zaidi kuliko kiwango kilichoidhinishwa na sekta ya mawasiliano duniani kwa mujibu wa na Jukwaa la Watengenezaji wa Simu za Mkononi (MMF).
Akizungumza kuhusu hatua ya Tigo kutoa tahadhari kwa wateja wake Zakaria alisema, ``Wanunuzi wanatakiwa kuwa waangalifu wakati wanaponunua simu mpya au vifaa vya mawasiliano madukani au katika intaneti kwa sababu bidhaa nyingi feki zinatengenezwa kwa kuigaa muundo na nembo za kibiashara za bidhaa halisi kwa makusudi ili kuwalaghai wateja.
``Ili kuweza kuelewa iwapo simu yako ni feki au ni halisi unatakiwa kupiga namba namba *#06# ambapo atapokea  namba ya IMEI ya simu hiyo na kisha kutima kwa njia ya jumbe mfupi kwenda namba 15090 ambapo utapata jibu iwapo simu hiyo ya mkononi ni halisi au ni bandia,” alisema Zacharia.



 Mwisho 
Mkuu wa  Kitengo cha Vifaa vya Mawasiliano wa TigoDavid Zakaria akielezea athari  za matumizi ya  simu bandia kwa waandishi wa habari  (Hawapo pichani) katika mkutano uliofanyika mapema leo katika makao makuu ya Tigo Kijitonyama Dar es salaam., kushoto kwake ni Meneja wa Mawasiliano, John Wanyancha


Dar es Salaam, Februari 16 2016 - Watumiaji wa simu za mkononi wameonywa dhidi ya matumizi ya simu bandia na zisisokidhi viwango vya ubora ambazo tayari zimetangwa kupigwa marufuku na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuanzia mwezi Juni mwaka huu.
Kutokana na sababu hiyo, Tigo, ambayo ni kampuni ya kidijitali, imeanza kuendesha kampeni ya kuhamasisisha wateja wake na umma kwa jumla kupitia vyombo vya Habari inayolenga kuwaepusha na athari za matumizi ya simu bandia.

 ``Kwa mujibu wa maelekezo ya TCRA matumizi ya simu za mkononi ambazo namba zake za utambulisho wa kimataifa (IMEI) ni bandia yatapigwa marufuku kutumika kwa mitandao yote ya simu nchini Tanzania kuanzia Juni 16 mwaka huu. Ili kujiepusha na usumbufu wowote utakaotokana na hatua hii tunawashauri wateja wetu kujipatia simu halisi na bora kutoka maduka ya Tigo yaliyo karibu nao,`` alisema Mkuu wa  Kitengo cha Vifaa vya Mawasiliano wa Tigo, David Zakaria.
Ripoti ya utafiti ulichapishwa katika tovuti ya GSMA ("http://www.gsma.com" www.gsma.com ) inasema kwamba tofauti na ilivyo kwa simu halali ambazo hupitia mamia ya hatua mbalimbali za kuhakiki ubora wake kabla ya kupelekwa sokoni, simu bandia hazifanyiwi majarbio ya ubora na kuna taarifa za kitafiti zinazoonyesha kuwa baadhi ya simu bandia zina kiwango kikubwa cha madini ya risasi na vitu vingine ambavyo ni hatari kwa mazingira na afya ya binadamu.
Ripoti hiyo inaendelea kusema kuwa simu feki zinatengenezwa na malighafi dhaifu zisizokidhi viwango na zimeshaonesha kuwa kiwango cha hatari cha vyuma na kemikali kama risasi hadi kufikia kiwango cha mara 40 zaidi kuliko kiwango kilichoidhinishwa na sekta ya mawasiliano duniani kwa mujibu wa na Jukwaa la Watengenezaji wa Simu za Mkononi (MMF).
Akizungumza kuhusu hatua ya Tigo kutoa tahadhari kwa wateja wake Zakaria alisema, ``Wanunuzi wanatakiwa kuwa waangalifu wakati wanaponunua simu mpya au vifaa vya mawasiliano madukani au katika intaneti kwa sababu bidhaa nyingi feki zinatengenezwa kwa kuigaa muundo na nembo za kibiashara za bidhaa halisi kwa makusudi ili kuwalaghai wateja.
``Ili kuweza kuelewa iwapo simu yako ni feki au ni halisi unatakiwa kupiga namba namba *#06# ambapo atapokea  namba ya IMEI ya simu hiyo na kisha kutima kwa njia ya jumbe mfupi kwenda namba 15090 ambapo utapata jibu iwapo simu hiyo ya mkononi ni halisi au ni bandia,” alisema Zacharia.



 Mwisho 

Tuesday 16 February 2016

Mabalozi wa Huawei wakipozi siku ya uzinduzi wa promotion ya Valentine ya wiki 3 inayoendeshwa na kampuni ya Huawei Tanzania uliofanyika mwishoni mwa wiki, Mlimani City Dar es Salaam.
Balozi wa Huawei akikabidhi zawadi kwa mteja siku ya uzinduzi wa promotion ya Valentine ya wiki 3 inayoendeshwa na kampuni ya Huawei Tanzania uliofanyika mwishoni mwa wiki, Mlimani City Dar es Salaam.
Balozi wa Huawei akikabidhi zawadi kwa mteja siku ya uzinduzi wa promotion ya Valentine ya wiki 3 inayoendeshwa na kampuni ya Huawei Tanzania uliofanyika mwishoni mwa wiki, Mlimani City Dar es Salaam.
Baadhi ya wateja wakipata picha ya ukumbusho na balozi wa Huawei siku ya uzinduzi wa promotion ya Valentine ya wiki 3 inayoendeshwa na kampuni ya Huawei Tanzania uliofanyika mwishoni mwa wiki, Mlimani City Dar es Salaam.
Balozi wa Huawei akikabidhi zawadi kwa wateja siku ya uzinduzi wa promotion ya Valentine ya wiki 3 inayoendeshwa na kampuni ya Huawei Tanzania uliofanyika mwishoni mwa wiki, Mlimani City Dar es Salaam.
Bw. Sylvester Manyara, Meneja Mwandamizi  Huawei Tanzania(Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wateja walioshiriki katika uzinduzi wa promotion ya Valentine ya wiki 3 inayoendeshwa na kampuni ya Huawei Tanzania.
Bw. Sylvester Manyara, Meneja Mwandamizi  Huawei Tanzania(Kushoto) akimkabidhi Mteja mfuko wa zawadi pamoja na kadi katika uzinduzi wa promotion ya Valentine ya wiki 3   inayoendeshwa na kampuni ya Huawei Tanzania uliofanyika mwishoni mwa wiki hii, Mlimani City Dar es Salaam.

Baadhi ya wateja wakipata maelezo kutoka kwa mabalozi wa Huawei siku ya uzinduzi wa promotion ya Valentine ya wiki 3 inayoendeshwa na kampuni ya Huawei Tanzania uliofanyika mwishoni mwa wiki, Mlimani City Dar es Salaam. 

Na Mwandishi wetu, 
Kampuni ya simu ya Huawei, inayoshika nafasi ya tatu kwa utengenezaji na uuzaji wa simu za mkononi ulimwenguni imezindua promosheni ya Valentine ya muda wa wiki 3 inayohusisha vitu mbalimbali ikiwa ni pamoja na utoaji zawadi kwa wanunuzi wa simu za Huawei kutoka kwenye maduka yao mbalimbali ya rejareja yaliyosajiliwa.
Promotion hiyo itahusisha simu kuu mbili ambazo ni Huawei P8 na Huawei G8. Zawadi zinazotolewa kwa wateja ni pamoja na “selfie sticks, spika za Bluetooth na T-shirts. Pamoja na zawadi zote hizo ,wateja hao pia wanapewa fursa ya kupata picha nzuri za kumbukumbu ili waweze kuzitumia kwenye mitandao ya kijamii kama instagram na mingine.
Kampeni hii Iliyozinduliwa wikiendi hii mjini Dar es Salaam eneo la  Mlimani City, inawaahidi wateja wa Huawei kuona thamani ya pesa yao kutokana na zawadi watakazopatiwa .
Kwa mujibu wa report ya simu za mkononi ya hivi karibuni nchini Tanzania ilivyochapishwa mwaka jana na mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA), idadi ya watanzania wanaotumia simu za mkononi, waliojisajili imeongezeka kwa asilimia 16 kwa mwaka 2014 kufikia milioni 31.86 hiyo ni sawa na asilimia 67 kwa watanzania wote wanaotumia simu.
Huawei Tanzania wanaahidi kuendelea kutatua uhitaji wa wateja wao kwa kuwapatia   simu zenye ubora wa hali ya juu na orijino.
Tunatarajia kutoa huduma bora ya mawasiliano na intanet kwa bei nafuu kwa wananchi na pia kuwazawadia wateja wetu wale wazamani na wapya,  vifaa bora na vya kisasa vitakavyoweza kuongeza wigo katika matumizi ya simu zao za smatiphone  na intaneti pia” alisema Bw. Peter Zhangjunliang, Meneja wa Huawei nchini Tanzania katika uzinduzi wa Promotion hiyo.
Akielezea promosheni hiyo, Bw. Peter Zhangjunliang alisema; promosheni hii ya wiki 3 ni ya nchi nzima na ipo wazi kwa watanzania wote watakao nunua simu za G8 na P8 kutoka Huawei.”

Huawei, rafiki yako kwa simu origino.

Kuhusu Huawei
Kampuni ya Huawei imejizatiti katika kutengeneza bidhaa bora kwa matoleo tofauti ulimwenguni, kutoa huduma rafiki za simu, kwenye intaneti kwa wateja wake. Kampuni ya Huawei inajulikana duniani katika utengenezaji wa simu za mkononi, huduma za intaneti na vifaa vya majumbani.
Mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 2015, bidhaa vya Kampuni ya Huawei zinapatikana  zaidi ya nchi 150 ulimwenguni kote. Huawei ni kampuni ya 3 katika usambazaji wa simu (2015) ikiwa imesambaza zaidi ya milioni 100 ulimwenguni. Kampuni ya Huawei imeanzisha ushirikiano  na makampuni makubwa duniani kama Tigo, Vodacom, Airtel, Zantel, Sasatel, TTCL, SmileCom, Safaricom, MTN, CellC, Telefónica, China Mobile, Vodafone, T-Mobile, BT, China Telecom, NTT Docomo, France Telecom, na China Unicom. 
Kwa maelezo zaidi tafadhali tembelea www.huaweidevice.com

dk kigwa9Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akitoa ufafanuzi juu ya Wizara yake kuhakikisha itapeleka Madaktari bingwa katika mikoa mbalimbali nchini ikiwemo hospitali hiyo ya Mkoa wa Ruvuma wakati wa ziara yake aliyoifanya mapema Februari 13.2016.

Kauli hiyo ya serikali imetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto mjini Songea, Dkt. Hamisi Kigwangalla baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma na kituo cha afya cha Mjimwema kilichopo mjini Songea huku akiitaka mikoa ya pembezoni ukiwemo mkoa huo wa Ruvuma kuweka mazingira ya kuwavutia madaktari bingwa kufanya kazi katika mikoa yao.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bw. Said Mwambungu amesema kuwa mkoa huo umeridhishwa na staili ya ziara ya kushtukiza na kwamba wanajitahidi kuboresha vituo vya afya vya Mjimwema Songea, Madaba na cha wilaya ya Namtumbo ili vipandishwe hadhi kuwa hospitali za wilaya.

Pia Dk. Kigwangalla alipata wasaha wa kutembelea maeneo mbalimbali ya Hospitali hiyo na kujionea utendaji wa kazi huku akitoa wito katika suala la maboresho zaidi.

Imeandaliwa na Andrew Chale wa Modewjiblog, Ruvuma.

dk kigwa4

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla (katikati) akijiandaa kuingia kukagua utendaji wa kazi na vifaa ndani ya chumba cha upasuaji cha Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma wakati wa ziara yake hiyo Februari 13.2016.

dk kigwa

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akijiandaa kuingia kwenye chumba cha upasuaji wakati wa ziara yake hiyo, aliyoifanya mapema Februari 13.2016.

dk kigws

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akiangalia moja ya vitanda vinavyotumika katika upasuaji hospitalini hapo ambapo hata hivyo aliambiwa changamoto kuwa baadhi ya taa za vitanda hivyo kuwa na hitilafu wakati ziara hiyo mapema Februari 13.2016. (Picha zote na Andrew Chale,modewjiblog-Songea, Ruvuma)

RC IringaMkuu wa mkoa wa Iringa Bi.Amina Masenza akitoa taarifa kwa Naibu Waziri wa Afya, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa kwanza waliokaa kushoto) wakati alipotembelea ofisini hapo. Wengine ni watendaji wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (waliokaa kulia).

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dk. Hamisi Kingwangalla mapema leo Februari 15, ametembelea kambi ya Wagonjwa wa Kipindupindu pamoja na wale waliokumbwa na mafuriko katika kijiji Mboliboli Kata Pawaga Wilayani Iringa ambapo hadi sasa kambi hiyo ina wagonjwa 40 huku zaidi ya wagonjwa 223 walilipotiwa kuugua tangu kipindupindu kimeanza katika eneo hilo.

Mkuu wa mkoa wa Iringa Bi.Amina Masenza wakati wa kutoa taarifa yake kwa Naibu Waziri Dk. Kigwangalla aliyetembea ya Mkuu wa mkoa huyo, alimweleza kuwa kati ya wagonjwa hao 223, wagonjwa 17 ni watoto walio na umri wa chini ya miaka 5, Mbali na hao hadi sasa yamesababisha kifo kimoja.

Ugonjwa huo umeelezwa kuwa umewakumba kutokana na mvua zilizonyesha na kubomoa vyoo na kutapanya kinyesi hali iliyopelekea ugonjwa huo kusambaa Zaidi katika makazi ya wananchi hao.

Hadi sasa eneo hilo limekumbwa na maji huku wananchi wakilazimika kuyakimbia makazi yao na hata kuzungukwa na maji karibu eneo kubwa na usafiri wa watoa huduma kuwa wa shida ikiwemo kutumia boti maalum ama chopa.

Mkoa huo ulikumbwa na mvua mnamo Februari 3 hadi leo bado maji yameendelea kuzingira maeneo ya vijiji hivyo.

Imeandaliwa na Andrew Chale, modewjiblog-Iringa.

RC Iringa

DSC_0468

Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akitoa taarifa namna ya kamati yake ilivyopambana usiku na mchana na hatua waliofikia katika kuakikisha kipindupindu kinakwisha katika eneo hilo huku wakiendelea na jitihada za kupambana na mafuriko ikiwemo kuokoa wananchi waliobakia eneo hilo.

kigwanga

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla, akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa mara baada ya kumaliza kwa mazungumzo na taarifa fupi juu ya ugonjwa wa kipindupindu kwenye maeneo ya vijiji vya Mkoa huo ambapo hadi leo wamefikia jumla ya wagonjwa 40.

dk kigwanomic

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Hamisi Kigwangalla pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela wakiwasili katika uwanja wa Ndege wa Nduli, Iringa tayari kwa kuelekea kupanda Chopa kuelekea kwenye maeneo yaliyokumbwa na mafuriko pamoja na ugonjwa wa kipindupindu.

dk kigwangaz

Wakielekea katika Chopa maalum ya jeshi la Polisi kwa ajili ya kuwafikia wananchi waliozingirwa na maji ya mafuriko pamoja na ugonjwa wa kipindupindu.

Dk kigwaziiNaibu Waziri wa Afya, Dk.Kigwangalla akipanda Chopa tayari kuelekea kwenye eneo lililokumbwa na mafuriko katika vijiji vya Mbolimboli, Pawaga, Mkoani Iringa. (Picha zote na Andrew Chale,modewjiblog-Iringa).

Monday 15 February 2016

 The  supporting  Syria  conference  in  London

The supporting Syria conference in London




The  supporting  Syria  conference  in  Londo

IMG_2143

Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu ametoa hisia zake kuhusu kuandikwa katika mitandao ya kijamii kupitia kipindi cha Power Breakfast kinachorushwa na Clouds Fm.

Unaweza kumsikiliza hapa chini wakati akizungumzia jambo hilo;


Gari aina ya NOAH Namba T378 BYH rangi nyeupe imekamatwa huko nachingwe mkoani lindi. Baada ya uchunguzi polisi wamebaini kuwa rangi ya awali ya gari hiyo ni TRIM na mmiliki wake halali ni ABDALA MOHAMED MCHONDA P.O.BOX 1370 DAR ES SALAAM. Namba original za gari ni T 223 CUX. Yeyote mwenye taarifa ya kupotea gari yenye maelezo hayo awasialiane na Polisi Nachingwea kupitia RTO LINDI [0658 376074].Imeandaliwa na RSA na Dj Sek


Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM, Kata ya Kirumba Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza, leo wamefunga Ofisi ya Taasisi ya Mikopo ya WADOKI (Wadoki Saccos) pamoja na Hotel ya KIRUMBA RESORT kutokana na watajwa kushindwa kulipia kodi ya pango.

Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kirumba Acheni Maulid (anaeongea pichani) amesema kuwa wanachama hao wamefikia maamuzi hayo kutokana na kutumia majengo ya CCM katika kata hiyo huku wakiwa hawalipii kodi.

Wanachama wa CCM katika Kata hiyo ya Kirumba wamesema kuwa, maamuzi yao yatatoa fundisho kwa wawekezaji wengine wanaotumia vitega uchumi vya Chama hicho katika maendeo mbalimbali nchini huku wakiwa hawalipii kodi ambapo wametahadharisha kwamba wale wote wenye hulka hiyo wajiandae kutumbuliwa (kuondolewa katika majengo hayo).

Katibu Mwenezi wa CCM Kata ya Kirumba Juma Wesa pamoja na Katibu wa Chama hicho Wilaya ya Ilemela Acheni Maulidi, wamesema kuwa maamuzi yaliyochukuliwa na wanachama hayo ni sahihi kwa kuwa malalamiko ya wawekezaji hao yaliishajadiliwa hadi ngazi za juu na kuonekana kwamba wawekezaji hao hawatii makubaliano yao ikiwemo kulipa kodi ya pango kwa wakati.

Meneja wa Kirumba Resort hakutaka kuzungumzia malalamiko hayo kwa madai kwamba mzungumzaji ni Mkurugenzi ambae alidai amesafiri huku Uongozi wa Wadoki Saccos ukishindwa kupatikana.
Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kirumba Acheni Maulid akitoa kwa wanaccm baada ya wanachama hao kufunga Ofisi ya Wadoki Kirumba pamoja na Hotel ya Kirumba Resort, hii leo
Katibu wa CCM Wilaya ya Ilemela, Acheni Maulidi akizungumza baada ya wanaccm kufunga Ofisi ya Wadoki Kirumba pamoja na Hotel ya Kirumba Resort, hii leo
Katibu Mwenezi wa CCM Kata ya Kirumba Wesa Juma, akizungumza baada ya wanaccm kufunga Ofisi ya Wadoki Kirumba pamoja na Hotel ya Kirumba Resort, hii leo
Jane Masso ambae ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa Kata ya Kirumba (kulia) amesema wanachama watahakikisha vitega uchumi vya chama vinatumika vyema kwa ajili ya maendeleo yao.
Mmoja wa wanaccm akizungumza baada ya wanaccm kufunga Ofisi ya Wadoki Kirumba pamoja na Hotel ya Kirumba Resort, hii leo
Mmoja wa wanaccm akizungumza baada ya wanaccm kufunga Ofisi ya Wadoki Kirumba pamoja na Hotel ya Kirumba Resort, hii leo
Wanachama wa CCM wakiwa nje ya Hotel ya Kirumba Resort, hii leo baada ya kuifunga kutoa huduma
Wanachama wa CCM wakiwa nje ya Hotel ya Kirumba Resort, hii leo baada ya kuifunga kutoa huduma
Wanachama wa CCM wakiwa nje ya Hotel ya Kirumba Resort, hii leo baada ya kuifunga kutoa huduma
Ofisi ya Wadoki Saccos Kirumba baada ya kuwekewa kama ishara ya kufungwa
Ulinzi wa Askari wa Kutuliza ghasia ulikuwepo ili kuhakikisha hakuna uhalibifu wowote ambao ungeweza kufanyika ambapo suala hilo limefikishwa Kituo cha Polisi Kirumba na kila upande unawasilisha vielelezo vyake ili kutambua wanaokiuka makubaliano ya mkataba wa upangaji.
Imeandaliwa na George Binagi-GB Pazzo @Binagi Media Group