Monday 13 May 2013



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhd5Q_Ix0Yry6AnEkm5iZ-11ESZYYmoLEox9vTnvJ_DLzLaGGsWNaOd6vtToFaftL92lstHFagPc9ekAwsAli1uOjEDBEcTOCdjVEJwGzLmdeTzBBuCRor_TpOULOzWXQHwHFg0Zd6cIy6H/s1600/images.jpg

Website: www.ccmuk.org, ccmuk.org/blog, Facebook – chama cha mapinduzi uingereza, Twitter CCM UK.

WATANZANIA WENGI JIJI LA CARDIFF-WALES (UK) WAJIUNGA NA CCM.
Katika ufunguzi huo Jumamosi tarehe 11 Mei 2013 ulijaa shamrashamra na nderemo na  kuhudhuriwa na viongozi wote wa Tawi la CCM UK, Mwenyekiti wa Tawi la CCM UNITED KINGDOM Ndg  Maina Ang'iela Owino, Makamu Mwenyekiti  Ndugu Said Sukwa, Katibu Bi. Mariam Mungula, Naibu Katibu Ndugu Albert Ntemi, Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi Ndugu Leybab Mdegela, Naibu Katibu Itikadi, Siasa na Uenezi Ndugu Abraham Sangiwa, Katibu wa Uchumi na Fedha Ndugu John Juma Lyimo, Naibu Katibu Uchumi na Fedha Ndugu Mohamed Upete na wanaCCM toka mashina mbalimbali ya CCM UK.
 Mwenyekiti wa Tawi la CCM UNITED KINGDOM Ndg  Maina Ang'iela Owino aliwashukuru Watanzania hao kwa kujitokeza kwa wingi kuandaa, kuyakubali madhumuni  na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi.  Ndg Owino  aliwakumbusha kuwa uhalali wa shina lao unajumuishwa katika Sera ya nje na matawi yake katika Katiba ya CCM.
Ndg Owino aliwakumbusha kuwa kujiunga na CCM kunaambatana na kuzingatia masharti ya kuheshimu watu, kufanya juhudi za kuielewa, kuielezea, kuitetea na kuitekeleza Itikadi na Siasa ya CCM. Pia kwamba CCM inathamini haki na wajibu wa mwanachama.
Aidha Ndg Owino hakusita kuwakumbusha kuwa CCM na Serikali yake inaendelea kujijenga na kuboresha taasisi zake ili kuendana na mahitaji ya kizazi na wakati uliopo na hivyo basi  wanaCCM Cardiff wasioneane haya wala kuogopa kuchagua viongozi wenye sifa za kutosheka na wasio tawaliwa na tamaa na watakao zingatia miiko ya uongozi kama inavyoainishwa katika katiba ya CCM.
Kabla ya kuhitimisha hotuba yake Ndg Owino alichambua na kuainisha kwa kina na kuishirikisha halaiki kufanya tathmini ya wazi ya jinsi CCM imeiongoza serikali kutekeleza ilani yake ya uchaguzi ya 2005/2010 na mafanikio dhahiri yanayopatika katika kutatua kero za wananchi. Aidha alisema baadhi ya changamoto zilizopo nchini ni matokeo ya mabadiliko endelevu, kukua na kuendelea kwa mifumo na taasisi za umma na sekta binafsi na kwamba CCM na serikali yake inaendele kujiimarisha kuyakabili kwa mikakati na mipango endelevu ya muda mfupi na mrefu, pia Ndugu Maina aliwakumbusha Wana CCM UK Kuwa mchango wao unathaminiwa na ni wamuhimu katika kuleta mabadiliko yatayowanufaisha wengi katika nyanja mbalimbali muhimu za kimaendeleo na kichumi
Idara ya Itikadi Siasa na Uenezi na ile ya Uchumi na Fedha walitoa machache yanayohusu idara zao na namna zinavyofanya kazi ili kuwapa mwanga wanachama wapya na viongozi katika shina hilo.
Ufunguzi huo ulifuatiwa na uchaguzi wa Viongozi mashina uliosimamiwa na Katibu wa CCM UK, Bi Mariam Mungula.
Viongozi waliochaguliwa katika shina hilo jipya la Cardiff – Wales ni;
  1. Chande Kigwalilo                    Mwenyekiti wa Shina
  2. Bi. Rosemary Kiputa              Katibu wa Shina
  3. Prudencia Kimiti                      Mjumbe wa Shina
  4. Munde Nyirambo                     Mjumbe wa Shina
  5. Alen  Mguto                             Mjumbe wa Shina
Mara baada ya uchaguzi huo Mwenyekiti wa shina jipya la Cardiff Ndugu Chande Kigwalilo alitoa machache na kushukuru wajumbe na wanachama kumpa nafasi ya kuliongoza shina na kushukuru uongozi wa tawi kwa kufanikisha ufunguzi huo na kuwakarakibisha Jijini Cardiff.

Imetolewa na Idara ya Itikadi Siasa na Uenezi
CCM TAWI LA UNITED KINGDOM