Sunday 20 October 2013

WAZIRI WA KILIMO, MHE. CHRISTOPHER CHIZA KUKUTANA NA WATANZANIA LONDON

Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Christopher Chiza 
Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania London unawakaribisha Watanzania wote watakaoweza kupata fursa kuja kuzungumza na Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Christopher Chiza na Wawakilishi kutoka SAGCOT hapo Ubalozini siku ya Jumatano (tarehe 23 Octoba 2013) kuanzia saa Kumi na Moja jioni (17:00).

Mheshimiwa Waziri anatarajiwa kuzungumzia masuala mbalimbali ya Kilimo, fursa zilizomo katika kilimo na ushirikishwaji wa Diaspora katika uwekezaji katika sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya nchi. Aidha Mhe. Christopher Chiza anatarajiwa kujibu maswali mbalimbali kutoka kwa wananchi watakaohudhuria mkutano huo.

IMETOLEWA NA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI UINGEREZA, LONDON