Wednesday 3 July 2013

TASWIRA: RAIS BARACK OBAMA NA RAIS KIKWETE WALIPOTEMBELEA MRADI WA SYMBION UBUNGO JIJINI DAR ES SALAAM.

TASWIRA: RAIS BARACK OBAMA NA RAIS KIKWETE WALIPOTEMBELEA MRADI WA SYMBION UBUNGO JIJINI DAR ES SALAAM.

 Rais Barrack Obama wa Marekani na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete  wakizungumza na watendaji wa kuu wa sekta ya umeme nchini.Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Mr.Maswi,mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Sadik Meck Sadik na watatu kushoto ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa  Sospeter  Muhongo wakati kiongozi huyo wa Marekani alipotembelea mradi wa kuzalisha umeme unaofanywa na kampuni ya Symbion power ya Marekani huko Ubungo jijini Dar es Salaam leo

TASWIRA ZA DHIFA YA KITAIFA ILIYOANDALIWA NA RAIS KIKWETE KWA AJILI YA RAIS WA MAREKANI BARACK OBAMA NA MKEWE MICHELLE OBAMA

 Rais Barack Obama wa Marekani na mkewe Michelle wakiangalia bendi ya polisi wakati wa dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho kikwete. Kushoto ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Serikali ya Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha Rais Barak Obama wa Marekani kwa Mawaziri wakuu wastaafu pamoja na viongozi wengine wakati wa dhifa ya kitaifa aliyomwandalia mgeni huyo Jumatatu usiku Ikulu jijini Dar es salaam, Pichani Akimsalimia Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha Rais Barak Obama wa Marekani kwa Mawaziri wakuu wastaafu pamoja na viongozi wengine wakati wa dhifa ya kitaifa aliyomwandalia mgeni huyo Jumatatu usiku Ikulu jijini Dar es salaam. Pichani akimsalimia Waziri Mkuu Mstaafu na Katibu mkuu mstaafu wa OAU Dr Salim Ahmed Salim
 Rais Barack Obama wa Marekani na mkewe Michelle wakiangalia ngoma za utamaduni pamoja na bendi ya polisi wakati wa dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho kikwete. Kushoto ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Serikali ya Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein.