Wednesday 18 December 2013

 Rais wa kwanza Mzalendo na Mpigania Uhuru wa Afrika Kusini, Nelson Mandela ‘Madiba’ akiwa ameshikilia viatu vyake ambavyo aliviacha nyumbani kwa Mzee Nsilo Swai alipoingia Tanzania kwa mara ya kwanza mwaka 1962 akitokea Afrika Kusini.

Mandela aliahidi kuvichukua viatu hivyo pindi atakaporejea Tanzania lakini katika safari hiyo ndipo alipoishia mikoni mwa makaburu wa Afrika Kusini na kumfunga kwa miaka 27.

Viatu hivyo aina ya Buti vilihifadhiwa hadi alipotoka na kukabidhiwa kwa Mandela na mjane wa Mzee Nsilo Swai, Bi Vicky Nsilo Swai (pichani kulia) mwaka 1995 Mandela alipotoka gerzani na hatim,aye kuwa Rais wa kwanza Mweusi wa Afrika Kusini.