Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi (wa pili kushoto) akiwa na 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mohamed Aboud 
walipotembelea eneo la tukio leo.Picha na Adrew Chale, Zanzibar
 Picha juu ni gari alilokua akitumia Paroko
 wa Kanisa la Katoliki Minara Miwili
Zanzibar, Evarist Mushi leo asubuhi likiwa limegonga ukuta muda mfupi 
baada ya watu wasiojuliakana kumshambulia Paroko Evarist Mushi kwa 
risasi na kufariki 
 Sehemu
 ya Waumini wakiwa wenye majozi muda mfupi baada ya kupata habari za 
kifo cha   Paroko wao wa  Kanisa la Katoliki Minara Miwili
Zanzibar, Evarist Mush kushambuliwa na risasi na watu wasiojulikana leo 
asubuhi  katika gari
lake wakati akienda kuendesha ibada ya saa 3.00
 Padri Cosmo Shayo(Kulia)akizungumza na viomgozi wa kanisa kuhusiana na tukio la  Paroko wa Kanisa la Katoliki Minara Miwili
Zanzibar, Evarist Mush kushambuliwa na risasi na watu wasiojulikana leo asubuhi  katika gari
lake wakati akienda kuendesha ibada ya saa 3.00
Picha
 juu na chini Sehemu ya waumini mbalimbali wakiwa nje ya viwanja vya 
hospitali ya mnazi mmoja leo asubuhi baada ya   Paroko wa Kanisa la 
Katoliki Minara Miwili
Zanzibar, Evarist Mush kushambuliwa na risasi na watu wasiojulikana leo 
asubuhi  katika gari
lake wakati akienda kuendesha ibada ya saa 3.00.Picha  Adrew Chale na Othman Maulid Othman-Shirika la Magazeti ya Serikali Zanzibar
Feb
17

 Katibu wa itikadi na uenezi wa ccm Nape Nnauye akizindua moja kati ya a mashina matatu aliyoyazindua leo

 MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Mkoa wa Dar es Salaam,  Ramadhan Madabida akizungumza

 Waziri wa Maji Prof Jummane Maghembe akiongea
 Aliyekua makamu mwenyekiti wa Bavicha Juliana Shonza akiongea 
Sehemu ya umati wa wa CCM
Mfuasi mmoja wa chadema akirudisha kadi na kujiunga tena na CCM.Picha na Adamu Mzee-Idara ya itikadi na Uenezi- CCM
---
Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Dar es salaam leo kimefanya mkutano mkubwa 
wa hadhara katika eneo la Goba, ambapo wananchama 162 wamejiunga leo, 
ambapo wapo wanachama wanne kutoka Chadema walijiunga hapo hapo.
Mgeni
 mualikwa katika shughuli hiyo alikuwa Katibu wa NEC ,Itikadi na Uenezi,
 ambaye licha ya kufungua mashina matatu ya chama, pia  aliwasaidia 
wakinana mama wa vikoba,shilingi milioni moja na pia kukabidhi pikipiki 
kwa vijana wa goba na kuahidi zingine kuwapatia karibuni.
Katika
 mkutano huo, Mtela Mwampamba na Juliana Shonza walipata nafasi ya 
kuzungumza na wananchi wa Goba na kuwaambia sababu zilizofanya kukihama 
Chadema,moja ni kutotenda haki na kuwa na siasa ya kibaguzi na 
chuki,vurugu na uchochezi na sio kutetea watu na maendeleo.
Saumu
 Kisena licha ya kufanya kazi na Chadema kwa miaka 9 lakini hajalipwa 
haki zake hivyo ameshangazwa kuona haki inahubiriwa nje wakati ndani 
hakuna chembe ya usawa.
Feb
17

Mbunge wa jimbo la Ubungo-Chadema na Mkurugenzi wa idara ya Habari na Uenezi -Chadema, John Mnyika
----
Kwa nyakati mbalimbali kuanzia mwezi Januari mpaka Februari 2013 
pametokea matatizo ya kuharibika kwa baadhi ya mitambo na kupungua kwa 
uzalishaji wa maji katika vyanzo vya mto Ruvu na hivyo kusababisha 
matatizo ya maji kwa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam na maeneo 
yanayohudumiwa na Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASA) katika Mkoa
 wa Pwani. 
DAWASA imeingia mkataba wa uendeshaji na Kampuni ya Maji Safi na Maji 
Taka Dar es Salaam (DAWASCO) wa kutekeleza majukumu mbalimbali ikiwemo 
kuendesha mitambo, kusimamia usambazaji wa maji na kufanya matengenezo 
na kutoa taarifa kwa wananchi kuhusu huduma zinazotolewa. Aidha, DAWASCO
 wanapaswa kuzingatia mikataba ya huduma kwa wateja ambayo inaitaka 
kutoa taarifa kwa umma pale kunapotokea matatizo ya maji. 
Kwa kuzingatia mikataba hiyo, DAWASA na DAWASCO wanapaswa kutoa 
matangazo kwa umma kuhusu matatizo mapya yaliyojitokeza mwezi Januari na
 Februari 2013 ili kuepusha matatizo hayo kuhusishwa na hatua ya 
kuwasilishwa na kuondolewa bungeni kwa hoja binafsi niliyoiwasilisha 
tarehe 4 Februari 2013 juu ya hatua za haraka za kuboresha upatikanaji 
wa maji safi na ushughulikiaji wa maji taka katika Jiji la Dar es 
salaam. 
Kwa wakazi wa Kibamba, Kwembe, Msigani, Mbezi, Saranga na Kimara ni 
muhimu wakatambua kwamba nimefuatilia na kujulishwa kwamba palikuwa na 
tatizo la kupungua kwa uzalishaji wa maji katika chanzo cha Ruvu Juu 
ambalo limerekebishwa tarehe 12 Februari 2013 hivyo maji yataendelea 
kupatikana kwa mujibu wa ratiba ya mgawo kama ilivyokuwa awali katika 
maeneo ambayo yalikuwa yakipata maji tangu mwaka 2012. 
Kwa wateja ambao bado watakuwa na matatizo katika maeneo yao 
wawasiliane na DAWASCO kupitia namba ya huduma kwa wateja 022 55 00 240 
au 0779090904 au info@dawasco.com ili hatua za haraka ziweze kuchukuliwa. 
Kwa wananchi wa Jiji zima la Dar es Salaam ambao maeneo yao yana mabomba
 yanayojulikana zaidi kama mabomba ya wachina ambayo hayatoi kabisa maji
 kwa miaka mingi na wale ambao maeneo yao hayana kabisa miundombinu ya 
mabomba ya maji; hatua za haraka kwa upande wao zinapaswa kutokana na 
utekelezaji wa hoja binafsi niliyowasilisha bungeni. 
Hali hii inayoendelea hivi sasa  ya DAWASA na DAWASCO kushindwa kufanya 
matengenezo ya mitambo kwa wakati na kushindwa kukabiliana na upungufu 
wa uzalishaji wa maji kwa ajili ya Jiji la Dar es Salaam kunathibitisha 
kwamba bunge lilipaswa kujadili hoja binafsi niliyoiwasilisha bungeni. 
Katika maelezo ya hoja pamoja na mambo mengine nilitaka Bunge ambacho ni
 chombo chenye wajibu wa kuisimamia serikali kwa niaba ya wananchi 
kurekebisha kasoro zilizopo katika utendaji na uwajibikaji wa Wizara ya 
Maji na vyombo vinavyohusika na utoaji na udhibiti wa huduma ya maji. 
Ifahamike kuwa majukumu ya utoaji wa huduma ya maji jijini Dar es salaam
 na baadhi ya maeneo ya Kibaha na Bagamoyo yanafanywa na Mamlaka ya 
Majisafi na Majitaka (DAWASA) ambayo ni mmiliki, mkodishaji na msimamizi
 wa utoaji wa huduma ya majisafi na maji taka na ina wajibu wa kupanga 
na kugharamia utekelezaji wa miradi ya miundombinu, kuiendeleza na 
kugharamia matengenezo ya dharura na makubwa. 
Mwaka 2005 DAWASA iliingia mkataba wa miaka kumi (10) wa uendeshaji na 
Shirika la Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASCO). Chini ya 
mkataba huo majumu ya DAWASCO ni kuendesha mitambo, kusimamia usambazaji
 wa maji na uondoshaji wa maji taka, kuuza maji kwa wateja , kutoa 
ankara kwa wateja, kukusanya maduhuli, kulipia gharama za uendeshaji, 
kutekeleza matengenezo makubwa yanayogharamiwa na DAWASA na kutekeleza 
uunganishaji wa maji kwa wateja wapya kwa kutumia mfuko wa maji. 
Kisheria na kimkataba DAWASA ina wajibu wa kuisimamia DAWASCO iliyoingia
 nayo mkataba; hata hivyo kwa kuwa yote ni taasisi na mashirika ya umma 
ambayo bodi zake na watendaji wake wakuu huteuliwa na mamlaka zile zile 
na kuripoti kwa watu wale wale, hali ambayo ina athari kwenye utendaji 
na uwajibikaji. 
Wakati umefika sasa wa mkataba huo kati ya DAWASA na DAWASCO kuwekwa 
wazi kwa umma; kufanyiwa tathmini ya miaka zaidi ya mitano iliyopita ya 
utekelezaji; kufanyiwa marekebisho kwa ajili ya kipindi kilichobaki na 
maandalizi kuanza ya mfumo bora unaopaswa kuanza kuandaliwa baada ya 
kuisha kwa mkataba huo mwaka 2015. 
Izingatiwe kuwa tarehe 10 Februari 2013 niliiwasilisha kwa wananchi na 
kutoa wiki mbili kwa Waziri wa Maji kujitokeza kwa umma na kutoa majibu 
aliyokwepa kuyatoa bungeni  na iwapo Waziri Prof. Jumanne Maghembe 
hatatoa maelezo nitaongoza maandamano ya wananchi kwenda Wizarani 
kuwezesha hatua kuchukuliwa. 
Imetolewa tarehe 15 Februari 2013 na: 
John Mnyika (Mb)
Feb
17
 Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya  Nchini Dr Emmanuel Nchimbi akitoka chumba cha 
habari cha  makao makuu ya jeshi la polisi kilimani zanzibar baada ya 
kuongea na Waandishi wa vyombo mbalimbali vya Habari leo asubuhi 
kufwatia tukio la kupigwa risasi leo asubuhi Paroko wa Kanisa la Katoliki Minara Miwili
Zanzibar, Evarist Mushi na kufariki dunia,Padri Evarist Mushi alivamiwa na watu wasiojulikana akiwa njiani anaenda kuendesha misa katika
Kanisa la Mt.Theresia eneo la Mtoni Zanzibar
 Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya  Nchini Dr Emmanuel Nchimbi akizungumza na 
Waandishi wa vyombo mbalimbali vya Habari leo asubuhi katika ukumbi wa 
makao makuu ya jeshi la polisi kilimani zanzibar kutoka na tukio la 
kupigwa risasi leo asubuhi kwa Paroko wa Kanisa la Katoliki Minara Miwili
Zanzibar, Evarist Mushi na kufariki dunia,Padri Evarist Mushi alivamiwa na watu wasiojulikana akiwa njiani anaenda kuendesha misa katika
Kanisa la Mt.Theresia eneo la Mtoni Zanzibar
Sehemu
 ya Waandihi wa Habari wa vyombo mbalimbali Zanzibar wakimsikiliza kwa 
Makini Waziri wa mambo ya ndani ya nchini Dr Emmanuel nchimbo(hayupo 
picha)alipokua akitoa taarifa ya serikali kufwatia kupigwa risasi leo 
asubuhi kwa Paroko wa Kanisa la Katoliki Minara Miwili
Zanzibar, Evarist Mushi na kufariki dunia,Padri Evarist Mushi alivamiwa na watu wasiojulikana akiwa njiani anaenda kuendesha misa katika
Kanisa la Mt.Theresia eneo la Mtoni Zanzibar
Feb
17

 Paroko wa Kanisa la Katoliki Minara Miwili
Zanzibar, Evarist Mushi 
--- 
Paroko wa Kanisa la Katoliki Minara Miwili
Zanzibar, Evarist Mushi amefariki dunia baada ya kupigwa risasi saa 1.00
asubuhi na kufariki kabla hajafika hospitali ya Mnazi Mmoja. 
Paroko huyu amepigwa risasi akishuka katika gari
lake wakati akienda kuendesha ibada ya saa 3.00 leo.
Padri Evarist Mushi amepigwa risasi kichwani na
kufa papohapo na watu wasiojulikana akiwa njiani anaenda kuendesha misa katika
Kanisa la Mt.Theresia eneo la Mtoni Zanzibar.
Msemaji wa Jeshi Polisi Zanzibar Inspekta
Mohamed Mhina amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na amesema kuwa padre huyo
ameuawa wakati akijiandaa kuingia kanisani akitokea kwenye gari yake ambapo
ndipo alipofikwa na umauti huo.
Jeshi la Polisi visiwani humo kupitia kwa Msemaji wake Mkaguzi wa Polisi, Mohamed Mhina limelaani mauaji hayo na na kusisitiza kuwa Jeshi limeanza msako mkali wa kuwabaini wauaji hao.
Hili ni tukio la pili kutokea Zanzibar ambapo
tukio la kwanza lilitokea kwa Padre Ambrose Mkenda kupigwa risasi na kujeruhiwa
na watu wasiojulikana.




Magari yaliyosababisha vifo hivyo vya watu tisa wakiwapo wanafunzi wa sekondari ya Chalinze mkoani Pwani










Rais
 Jakaya Mrisho Kikwete akifariji ndugu, jamaa na marafiki wa familia 
zilizoondokewa na watoto na wazazi kufuatia ajali ya barabarani maeneo 
ya kijiji cha Kibiki, Ubena Zomozi katika mkoa wa Pwani Februari 11, 
2013 iliyoua hapohapo watu wanane wakiwemo wanafunzi wa Shule ya 
Sekondari ya Chalinze baada ya gari dogo aina ya Toyota Mark II 
lililokuwa limebeba abiria wanane kugongana uso kwa uso na roli.Picha na IKULU
---
Rais Jakaya Mrisho Kikwete Jumamosi hii
 ya Februari 16, 2015 amekwenda kuhani na kufariji ndugu, jamaa na 
marafiki wa familia zilizoondokewa na watoto na wazazi kufuatia ajali ya
 barabarani maeneo ya kijiji cha Kibiki, Ubena Zomozi katika mkoa wa 
Pwani iliyotokea Februari 11, 2013 na kupoteza  hapohapo maisha ya watu 
tisa wakiwemo wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Chalinze baada ya gari 
dogo aina ya Toyota Mark II lililokuwa limebeba abiria wanane kugongana 
uso kwa uso na roli la mizigo
Familia alizokwenda kuhani na kuzifariji ni pamoja na za marehemu Hassan Erasto Kurunge (57), Maria Sadiki ((52) na mtoto wa mwaka mmoja Samweli Ismail wa kata ya Ubena.
Wengie ni marehemu Essau Enos Mwamgingo (16) , Stella Isaack Kazimoto (18), Bahati George Mbena (17) na Latifa Maneno (17) 
Akiwa ameongozana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe Mwantumu Mahiza na Mkuu 
wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Ahmed Kipozi, Rais Kikwete alieleza 
kusikitishwa kwake kwa ajali hiyo, na kuwataka madereva wawe makini 
katika kuzingatia sheria za usalama barabarani
Rais Kikwete alisikitishwa zaidi kwa taarifa kwamba gari hilo dogo 
lilikuwa limebeba abiria wanane, na kuwa  dereva wake ambaye pia 
alipoteza maisha, hakuwa makini katika kuzingatia sheria za usalama 
barabarani.
 
 







 
