Sunday 3 February 2008


salamu za lipumba kwa jk

Taarifa ya Mhe Profesa Lipumba juu ya Uteuzi wa Mhe Jakaya Kikwete kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa AU
Directorate of Information and Policy Dissemination
The Civic United Front (CUF)
Party Headquarters
P.O. Box 3637
Zanzibar
Tanzania
Tel. (+)255 (0)747 414100
(+)255 (0)741 257 665
E-mail: cufhabari@yahoo.com
Website: http://www.cuftz.org/Kufuatia kuchaguliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), Mwenyekiti wa Taifa wa CUF, Mheshimiwa Prof. Ibrahim Lipumba, ametoa taarifa ifuatayo:
“Nachukua nafasi hii kumpongeza kwa dhati kabisa Rais Jakaya Kikwete kwa heshima kubwa aliyopewa na viongozi wenzake wa nchi za Afrika waliyomchagua kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) kwa mwaka huu wa 2008.
Chama Cha Wananchi (CUF) kimezipokea habari hizo kwa furaha kubwa na kinaiona heshima hiyo ni ya Tanzania na Watanzania wote kama Taifa bila ya kujali itikadi zetu za kisiasa. Hapana shaka kwamba kuchaguliwa kwa Rais Kikwete kuuongoza Umoja huo kutasaidia kuzidi kuipandisha chati Tanzania na kuitangaza kimataifa.
Pamoja na kuwa ni heshima kubwa kwa Rais wetu na kwa nchi yetu, hatua hii inatupa changamoto zaidi kuzidi kuling’arisha jina la Tanzania katika bara la Afrika na ulimwengu wa kimataifa kupitia nyanja zote za kisiasa, kiuchumi na kijamii.
Natoa wito kwa Rais Jakaya Kikwete kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa mfano katika ujenzi wa demokrasia ya kweli kwa kujenga taasisi imara zitakazohakikisha sauti ya wananchi inasikika, maamuzi yao yanaheshimiwa na uwajibikaji unaimarika.
Katika uchumi, Tanzania iwe mfano katika kuhakikisha tunatumia rasilimali zetu nyingi na za kutosha kwa maslahi ya nchi yetu na watu wake kwa kujenga uchumi imara wa soko huria linalotoa ajira, tija na neema kwa wananchi wote. Na katika masuala ya kijamii, Tanzania iwe mfano katika kufikia malengo ya milenia.
Hii pia ni nafasi adhimu ya kukamilisha mazungumzo ya CCM na CUF ya kuupatia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa Zanzibar ili kumpa nafasi Rais Kikwete ya kushughulikia vyema migogoro mingine ya kisiasa barani Afrika, ambalo litakuwa sehemu muhimu ya majukumu yake akiwa Mwenyekiti wa AU.
Namhakikishia Rais kuwa mimi binafsi na Chama cha CUF tutampa kila ushirikiano na msaada anaouhitaji katika kutimiza matumaini ya Waafrika wenzetu waliotuamini kuuongoza Umoja wa Afrika. Kwa mara nyengine tena, tunasema hongera Rais Kikwete.
DAR ES SALAAM
1 Februari, 2008

© Michuzi Tarehe: 2.2.08



LAUNCHING AFRICAN WOMEN’S WEEK &
CONFERENCE ON AFRICAN FAMILY LIFE IN THE UK

THEME: “The impact of extended Family Pressure on families in the UK”
HOSTED BY: His Worshipful Cllr Bob Skelly, Mayor of Southwark
DATE: 13th March 2008
VENUE: Southwark Town Hall, Peckham Road London SE5 8UB
TIME: 6 – 9pm
CHAIR: Prof. Michal Lyons
Faculty of Arts and Human Sciences
London South Bank University




SPEAKERS:
Chair’s opening speech:

Professor Michal Lyons
Keynote Address:

Ms Alice Ukoko
Concerns over Child Protection/ Development
Within the African Community:

Mr Paul Angeli
Mental Health within the African community:

Dr Olajide Consultant Psychiatrist
International Trafficking:

Dr Carrie Pemberton

Moderator Interactive Session:

Mrs Sarah McCulloch
Panellists will include Politicians and Policy decision makers.