WAZIRI
 Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye, ametoa dukuduku lake la moyoni akisema 
hana uhasama na Waziri Mkuu aliyejiuzulu Edward Lowassa na kubainisha 
kuwa rushwa ya kimtandao iliyokighubika Chama cha Mapinduzi (CCM), ndiyo
 iliyomwangusha wilayani Hanang’. 
Sumaye ambaye amepigwa mweleka kwenye uchaguzi wa ujumbe wa Halmashauri 
Kuu (NEC) Taifa kupitia wilayani Hanang’ na Waziri wa Nchi, Ofisi ya 
Rais (Uwekezaji na Uwezeshaji), Mary Nagu, alikutana na wanahabari 
kuelezea mwendo mzima wa uchaguzi huo na hatima ya CCM. 
Akizungumza kwa kujiamini huku akinukuu kauli zake za nyuma kuhusu 
mwenendo wa rushwa ndani ya chama chake, alisema uchaguzi wa Hanang’ 
ulighubikwa na matumizi makubwa ya rushwa, vitisho vingi, uharamia wa 
kuhamisha wapiga kura usiku na maovu mengineyo mengi. 
“La msingi ni kuwa mimi sijakata na wala sitakata rufaa ya kupinga 
matokeo wala kupeleka malalamiko katika chama changu kwa sababu 
yaliyokuwa yakitendeka yalikuwa yanafahamika,” alisema. 
Katika kile kinachoweza kutafsiriwa kama kuondoa uvumi uliokuwepo kuwa 
Sumaye na Lowassa wana ugomvi wa kisiasa hasa wakati huu wa kujipanga 
kuelekea mbio za urais 2015, kiongozi huyo alisema hajazungumza na mtu 
kuhusiana na mambo hayo. 
Sumaye alisema taarifa hizo zimekuwa zikisambazwa na kunukuliwa kuwa 
zimetoka kwenye chanzo kilicho karibu naye, lakini akafafanua kuwa 
hawezi kupambana na Lowassa kwa sababu hana uhasama naye. 
“Nikiamua kugombea urais sitagombea kwa sababu ya mtu fulani bali 
nitagombea kwa sababu ya nchi na wananchi wa Tanzania,” alisema. 
Akifafanua kuhusu vitendo vya rushwa ndani ya CCM, alisema kuwa nchi 
nyingi hasa zenye demokrasia changa kama Tanzania zimeingia katika 
vurugu na kuhatarisha amani na utulivu nyakati za uchaguzi. 
Sumaye alisema madaraka yatakuja tu kama wananchi wapiga kura wanaona 
wewe ndiye utayewafaa na wala wasirubuniwe kwa fedha au jambo lolote kwa
 kutumia vibaya nafasi ya umaskini wao. 
“Hivi leo tunavyoongea hali ya rushwa wakati wa uchaguzi imekuwa mbaya 
zaidi. Katika uchaguzi wa kidemokrasia wapiga kura humchagua mwakilishi 
wanayemtaka kwa sababu ya uwezo wake yaani humchagua mwakilishi wao kwa 
ajili yao. 
“Katika demokrasia iliyopondeka kwa rushwa, fedha huwachagulia watu 
mwakilishi kwa ajili ya waliotoa fedha. Wapiga kura ni wapiga mihuri 
tu,” alisema. 
Sumaye bila kutaja majina ya wahusika, alisema hali imetoka kwenye 
kuhonga ili achaguliwe katika eneo lake na badala yake kuna rushwa za 
kimtandao ambapo mtu hutoa fedha katika maeneo mbalimbali nchini ili 
watakaochaguliwa wawe wafuasi wake mbele ya safari atakapowahitaji. 
“Uchaguzi huu umeghubikwa sana na matumizi makubwa ya fedha za rushwa. 
Suala la rushwa katika nchi yetu na katika CCM siyo mgeni lakini sasa 
tatizo hilo limeota mizizi na linazidi kuwa kubwa,” alisema. Kuhusu kwenda CHADEMA
 
Sumaye alikanusha vikali akisema hajawahi kukutana na kiongozi yeyote wa CHADEMA wala chama chochote cha upinzani. 
Lakini akabainisha kuwa hawapaswi kufikia kudai kuwa vyama vya upinzani au viongozi wake ni maadui wa CCM. 
“Mimi ningekuwa nimekutana nao ningesema tu mbona hata hao wengine 
wanaoutafuta urais kwa udi na uvumba huwa wanakutana nao? Alihoji. 
Alisema yeye ni mwanachama mwaminifu wa CCM na kwamba alishawahi kusema 
kuwa hayuko kwa ajili ya cheo na wala kukosa ujumbe wa NEC na hasa kwa 
njia iliyotumika hakumnyimi usingizi wala hahuzuniki kugombea urais kwa 
tiketi ya CCM endapo ataamua kufanya hivyo. 
Sumaye alisema kama ni matatizo, vyama vyote vina kasoro zake, hivyo 
haoni kama kuhama chama ni suluhu na kutamba kuwa kushindwa kwake 
kumempa nguvu zaidi na hivyo akiamua kugombea urais lazima apitie CCM. Kuhusu TAKUKURU
 
Alipoulizwa kuhusu utendaji wa Taaasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
 (TAKUKURU) kama imetimiza wajibu wake kushughulikia tuhuma za rushwa 
kwenye uchaguzi wilayani Hanang’, Sumaye alitafakari kidogo kisha 
akajibu kwa kutumia mfano. 
“Hivi kama nyie wanahabari mmekuja hapa mkanisikiliza haya 
ninayowaeleza, halafu kesho watu wanasoma kwenye magazeti yenu hawakuti 
kitu au kwenye televisheni hawaoni, wanaweza kusema mmetimiza jukumu 
lenu? Alihoji Sumaye. 
Kada huyo aliwaachia wanahabari watafsiri wenyewe kama kweli TAKUKURU 
inatimiza wajibu wake katika kushughulikia madai ya rushwa kwenye 
chaguzi. 
“Napenda nitambue kuwa haya ninayoyasema si matamu masikioni mwa baadhi 
yetu lakini ni vema tukayasikiliza kwa makini na kuchukua hatua chanya 
ili yasilete madhara zaidi katika jamii na wala tusidiriki 
kuwanyamazisha wanaoyazungumzi |  
 
 
 |